Posts

Showing posts from June, 2026

Seneta Miraj Abdillahi Apongeza juhudi za serikali katika Kupambana na Mihadarati Mombasa.

Image
  Seneta Mteule katika kaunti ya Mombasa Miraj Abdillahi amepongeza idara za usalama kwa juhudi zake za kupambana na matumizi ya mihadarati pamoja na kuimarisha usalama katika Kaunti ya Mombasa, hatua ambayo amesema imechangia kupungua kwa visa vya uhalifu na utovu wa usalama vilivyokuwa vikishuhudiwa katika maeneo mbalimbali ya kaunti hiyo. Amesema mafanikio hayo yametokana na ushirikiano mzuri kati ya vyombo vya usalama na wananchi. Akizungumza katika eneo bunge la Jomvu wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Kupambana na Dawa za Kulevya, Miraj amesema ukanda wa Pwani kwa miaka mingi umekuwa ukikabiliwa na changamoto ya matumizi na biashara ya mihadarati. Hata hivyo, amebainisha kuwa kupitia ushirikiano kati ya Wizara ya Usalama wa Ndani, vyombo vya usalama na serikali ya kaunti, hatua kubwa zimepigwa katika kudhibiti tatizo hilo. Amesema juhudi hizo zimewaokoa vijana wengi kutoka katika uraibu wa dawa za kulevya na kuwapa fursa ya kujijenga upya na kuboresha maisha yao....

Serikali ya Kaunti ya Mombasa Yaonya Wanaojenga Bila Kuzingatia Sheria

Image
                            Serikali ya Kaunti ya Mombasa imeanzisha operesheni ya kukabiliana na miradi yote ya ujenzi inayoendelea bila kuzingatia masharti ya vibali na sheria za mipango ya  mji, ikisema hatua hiyo inalenga kuimarisha usalama wa umma na kuhakikisha maendeleo yanafanyika kwa utaratibu. Kupitia taarifa iliyotolewa na wizara ya Ardhi, Mipango Miji, Makazi na Serikali Mitaani ikiongozwa na waziri Mohamed Husein Amadoh amesema kaunti hiyo imebaini ongezeko la miradi isiyofuata masharti ya vibali vya ujenzi pamoja na matakwa mengine ya kisheria, hali inayotishia usalama wa wananchi, mazingira na mpangilio wa miji.                                  Akisema licha ya kutoa notisi na maonyo kwa waendelezaji wa miradi na wamiliki wa majengo, baadhi yao wameendelea na shughuli za ujenzi kinyume cha s...

Wito wa Ushirikiano Watolewa Katika Vita Dhidi ya Mihadarati Nchini.

Image
                                Huku ulimwengu ukiadhimisha siku ya kupinga matumizi na ulanguzi wa dawa za kulevya,hapa Mombasa siku hiyo imeadhimishwa katika eneo bunge la Jomvu katika kituo cha Miritini huku viongozi wakionya kuwa taifa linakabiliwa na dharura ya kitaifa kutokana na ongezeko la matumizi ya dawa za kulevya,wito ukitolewa kwa serikali za kaunti pamoja na serikali ya kitaifa kushirikiana kwa karibu ili kuimarisha vita dhidi ya mihadarati . Kulingana na utafiti wa hivi karibuni wa kitaifa uliofanywa na Mamlaka ya Kitaifa ya Kupambana na Matumizi ya Pombe na Dawa za Kulevya (NACADA), takriban Wakenya milioni 4.7 wenye umri wa kati ya miaka 15 na 65 wanatumia angalau aina moja ya dawa za kulevya au kilevi. Utafiti huo unaonyesha kuwa eneo la Pwani lina kiwango cha juu zaidi cha matumizi ya dawa za kulevya nchini kwa asilimia 29.3, huku Kaunti ya Mombasa ikiongoza kwa kiwango cha asilimia 34...

KUPPET Yaitaka Serikali Kuboresha Ustawi wa Walimu na Ufadhili wa Shule.

Image
                            Chama cha Walimu wa Sekondari na Vyuo vya kadri (KUPPET) kimetoa wito wa kufanyika kwa mageuzi muhimu katika sekta ya elimu, ikiwemo kupandishwa vyeo kwa walimu,kuboreshwa kwa huduma za matibabu Kwa walimu na utoaji wa fedha za shule kwa wakati, pamoja na kushughulikia kwa kina visa vya ghasia shuleni. Akiongea wakati wa kongamano la 49 la walimu wakuu WA shule nchini KESSHA naibu katibu  mkuu wa KUPPET Moses Nthirima ametoa wito huo akisema kuwa shule imara zinajengwa kupitia uongozi,ushirikiano, msaada wa kutosha kwa walimu na utekelezaji wa sera bora za elimu. Amepongeza mapitio ya hivi karibuni ya Mwongozo wa Maendeleo ya Kazi kwa Walimu (CPG), akiyataja kuwa hatua muhimu katika kuboresha taaluma ya ualimu. Amesema kuwa kuanzishwa kwa njia mbili za maendeleo ya taaluma, ya kiutawala na ya darasani, pamoja na fursa za kuhama kati ya njia hizo, kutasaidia kupunguza hali y...

Wafanyabiashara wadogo 3000 kufaidika na mafunzo na fedha kutoka kwa Benki ya Absa na Google Hustle Academy.

Image
                                                         Benki ya Absa Kenya PLC kwa ushirikiano na Google Hustle Academy wametangaza ushirikiano wa kimkakati unaolenga kutoa mafunzo ya biashara na msaada wa kifedha kwa wafanyabiashara wadogo (SMEs) 3,000 nchini katika kipindi cha miezi 12 ijayo. Mpango huo unalenga kuwafikia na kuwawezesha wafanyabiashara kwa kuwapa ujuzi wa kidijitali, maarifa ya kifedha, mikakati ya kukuza biashara pamoja na mwongozo wa kurasimisha na kupanua shughuli zao kwa njia endelevu.Kufikia sasa, programu hiyo imefaidi makundi matatu ya mafunzo yaliyohudhuriwa na zaidi ya wafanyabiashara 600. Akizungumza kuhusu ushirikiano huo, Mkurugenzi wa Huduma za Biashara wa Absa Bank Kenya, Renato D’Souza, amesema benki hiyo imejitolea kuwawezesha wafanyabiashara kwa kuwapatia zana na rasilimali wanazohitaji kufanikiwa. “T...

Zaidi ya walimu wakuu 10,000 wa shule za sekondari kukongamana Mombasa katika warsha ya kila mwaka.

Image
Muungano wa Walimu Wakuu wa Shule za Sekondari nchini (KESSHA) umeanza Kongamano lake la 49 la Kitaifa la KCB/KESSHA katika Ukumbi wa Sheikh Zayed kaunti ya Mombasa, likiwakutanisha wakuu wa shule za sekondari kutoka maeneo mbalimbali nchini kujadili mustakabali wa elimu na utekelezaji wa Elimu ya Umilisi (CBE) huku zaidi ya walimu wakuu elfu kumi wakitarajiwa kuhudhuria. Kongamano hilo la siku tano linaongozwa na kaulimbiu ya “Shule Imara na Uongozi wa Ushirikiano kwa Kuendeleza Elimu ya Umilisi.” Akizungumza katika mkutano na wanahabari kabla ya kuanza kwa kongamano hilo, Mwenyekiti wa Kitaifa wa KESSHA, Willie Kuria, amesema kaulimbiu hiyo inaakisi dhamira ya chama hicho ya kuimarisha uongozi wa shule, kuendeleza ushirikiano kati ya wadau wa elimu, na kuhakikisha utekelezaji wenye mafanikio wa Elimu ya Umilisi nchini. Kuria amesisitiza kuwa mageuzi ya sekta ya elimu yanahitaji ...

Spika wa bunge la kitaifa Moses Wetang’ula Akemea Siasa za Ukabila na Vurugu.

Image
                                                                                                            Spika wa Bunge la Kitaifa, Moses Wetang'ula, amewataka Wakenya kujiepusha na siasa za ukabila na kukumbatia umoja wa kitaifa, akisema mustakabali wa nchi unategemea viongozi na wananchi kuweka maslahi ya taifa mbele badala ya tofauti za kikabila na kisiasa. Akizungumza katika eneo la Likoni, Kaunti ya Mombasa, wakati wa hafla ya kuchangisha fedha kwa ajili ya Shirika la Kijamii la Salute (Salute CBO), Wetang'ula amesema maendeleo ya Kenya yatawezekana kupitia umoja, mshikamano na kuheshimu demokrasia. "Nchi yetu ni kubwa kuliko mtu yeyote, na uongozi hutoka kwa Mungu. Lengo letu linapaswa kuwa kuunganisha t...

Vijana Mombasa Wanufaika na TukTuk Kutoka Kwa Mission Relief Africa Kukabiliana na Ukosefu wa Ajira

Image
                             Vijana 25 kutoka familia zisizojiweza katika Kaunti ya Mombasa wamepokea TukTuk kupitia mpango wa kuwawezesha kiuchumi ulioanzishwa na Mission Relief Africa, hatua inayolenga kukabiliana na changamoto ya ukosefu wa ajira miongoni mwa vijana. Akizungumza wakati wa hafla ya ugawaji wa TukTuk hizo, Mwenyekiti wa Mission Relief Africa, Said Mabruk, alisema shirika hilo lilianzisha mpango huo ili kukabiliana na changamoto za kiuchumi zinazowakabili vijana wengi pamoja na ukosefu wa nafasi za ajira.                                Amesema Mission Relief Africa, ambayo ni tawi la Mission Relief UK nchini Kenya, imejijengea sifa kupitia shughuli mbalimbali za kibinadamu zikiwemo usambazaji wa chakula kwa familia zenye mahitaji, ugawaji wa nyama wakati wa Eid, misaada ya dharura kwa maeneo...

Mahafala 341 Wahitimu Kozi za utabibu katika Mahafali ya 19 ya chuo cha North Coast Medical Training College.

Image
                                         Jumla ya mahafala 341 wamefuzu katika vitengo mbalimbali katika taaluma ya utabibu na udaktari katika chuo cha north coast medical training college katika mahafali ya 19. Akiongea wakati wa hafla hiyo katibu mkuu wa chuo hicho Ruben Waswa amesema chuo hicho kimeendelea kupiga hatua kubwa za maendeleo, kikisajili ongezeko la idadi ya wahitimu kila mwaka kutokana na ubora wa mfumo wake wa elimu na mafunzo. Ameibainisha kuwa kozi za utabibu zinazotolewa na chuo hicho zinawapa wahitimu fursa kubwa za kupata ajira kwa haraka nchini na katika soko la kimataifa.                                           Aidha, amewahimiza wazazi na walezi kuwapeleka watoto wao katika vyuo vinavyotambuliwa na kutoa mafunzo bora ili kuwawezesha kupata elimu st...

Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Kisiasa Yawapa Walemavu Mafunzo ya Masuala ya Uchaguzi.

Image
                                                              Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Kisiasa nchini imeandaa mafunzo maalum ya maandalizi ya uchaguzi kwa walemavu katika Kaunti ya Mombasa, yakilenga kuwajenga uwezo, kuwafahamisha haki zao na kuongeza ushiriki wao katika mchakato wa uchaguzi. Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, mratibu kutoka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Kisiasa katika kaunti ya Mombasa Suzan Mwaingo amesema lengo kuu ni kuwahamasisha walemavu kujiunga na vyama vya kisiasa na kufahamu namna wanavyoweza kupata nafasi za uongozi kupitia uteuzi wa vyama. Akisema ofisi hiyo imejipanga vyema kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2027 na imeendelea kushirikiana na Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) kutoa elimu kuhusu sheria za uchaguzi na umuhimu wa kuzingatia sheria hizo ili kuepuka adhabu. Suzan amebainisha kuwa vyama 48 k...

Kenya Yasisitiza Ushirikiano wa Kimataifa katika Kuhifadhi Bahari.

Image
  Serikali ya Kenya imetoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kuchukua hatua za haraka na madhubuti kulinda mifumo ya ikolojia ya bahari na kuimarisha uchumi samawati wakati viongozi na wadau kutoka mataifa mbalimbali wakikutana katika Our Ocean Conference linalofanyika kaunti ya Mombasa. Akizungumza wakati wa ufunguzi rasmi wa kongamano hilo katika Hoteli ya PrideInn,naibu wa rais Kithure Kindiki amesema uhusiano wa Afrika na bahari ni wa kihistoria, wa kina na wa kudumu, akibainisha kuwa pwani, bandari na mifumo ya ikolojia ya bahari imekuwa msingi wa ustawi wa jamii nyingi kwa karne nyingi kupitia biashara, utamaduni na uchumi.                                             Amesema uchumi wa bahari duniani kwa sasa unakadiriwa kuwa na thamani ya takribani dola trilioni 3.3 za Marekani kwa mwaka, sawa na asilimia 2.5 ya pato la taifa la dunia, huku ukitarajiwa kufikia dola tr...

Maadhimisho ya Siku ya Mtoto mwafrika: Viongozi Kilifi watoa Wito wa Kulinda Watoto.

Image
                                                         Viongozi wa Kaunti ya Kilifi wametoa wito kwa jamii kushirikiana katika kuimarisha ulinzi wa watoto na kuhakikisha wanapata haki zao za msingi, ikiwemo elimu, huduma za afya, maji safi na mazingira salama ya kuishi. Wakizungumza wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa mwafrika, viongozi hao walisisitiza kuwa jukumu la kulinda watoto si la serikali pekee, bali ni wajibu wa kila mwanajamii.                                                           Akiongea katika hafla hiyo naibu Gavana wa Kilifi, Flora Chibule, amesema maadhimisho hayo yanatoa fursa ya kutafakari wajibu wa pamoja wa kulinda, kulea na kuwekeza kwa kila mtoto ili kuhakikisha...

Waziri Amadoh Awahimiza Wakazi wa Mwakirunge Kuunga Mkono Miradi ya Maendeleo.

Image
                                                                                                                Huku uchaguzi mkuu wa mwaka 2027 ukizidi kukaribia na siasa zikipamba moto katika Kaunti ya Mombasa, Waziri wa Ardhi, Makao na Ustawi wa Jiji la Mombasa, Mohammed Hussein Amadoh, amewatahadharisha wakazi wa kaunti hiyo dhidi ya kuhadaiwa kisiasa na kushawishiwa kupinga miradi mbalimbali ya maendeleo. Akizungumza katika kikao na wakazi wa eneo la Guu Ng'ombe-Mwakirunge, katika Eneo Bunge la Kisauni, Amadoh amesema ni muhimu kwa wananchi kuwa makini na kauli zinazotolewa na viongozi wa kisiasa, hasa kuhusu masuala ya maendeleo na umiliki wa ardhi. Amesisitiza kuwa wananchi wanapaswa kuunga mkono mir...