Kaunti ya Wajir yaandaa Sherehe za Madaraka Day kwa mara ya kwanza tangu Kenya ipate Uhuru.
Kaunti ya Wajir imeandika historia kwa kuandaa sherehe za 63 za Madaraka Day kwa mara ya kwanza tangu Kenya ipate uhuru. Serikali imesema hatua hiyo inaonyesha dhamira ya kuhakikisha maendeleo na shughuli za kitaifa zinafikia maeneo yote ya nchi huku zikikuza umoja, usawa na mshikamano wa kitaifa. Akizungumza katika mkutano na wanahabari kuelekea maadhimisho hayo, Msemaji wa Serikali, Isaac Mwaura , amesema kuwa tukio hilo linaonyesha dhamira ya serikali katika kukuza ushirikishwaji, usawa na mshikamano wa kitaifa. Alibainisha kuwa licha ya changamoto za uchumi wa dunia, ikiwemo athari za mgogoro unaoendelea Mashariki ya Kati, uchumi wa Kenya umeendelea kuwa thabiti na hivyo kuwezesha serikali kuendelea kuwekeza katika maendeleo na umoja wa kitaifa. Maandalizi ya sherehe hizo yameleta mabadiliko makubwa katika mji wa Wajir, ikiwemo ujenzi wa uwanja wa kisasa wenye uwezo wa kuhudumia zaidi ya watu 10,000, ubo...