Serikali Yaweka Zaidi ya Bilioni 721katika Ujenzi wa Nyumba za Bei Nafuu.
Serikali imewekeza fedha ya takriban Shilingi bilioni 731.5 katika mikataba ya ujenzi wa zaidi ya nyumba 280,000 zinazoendelea kujengwa katika maeneo mbalimbali nchini kupitia Mpango wa Nyumba za Bei Nafuu. Akizungumza wakati wa ufunguzi rasmi wa kongamano la Kila mwaka la chama Cha wasanifu mijengo nchini AAK 2026 iliyofanyika Diani, Kaunti ya Kwale, Kaimu Katibu wa Nyumba katika Idara ya Serikali ya Nyumba na Maendeleo ya Miji QS Cassius Kusienya, MBS,akiwakilisha na kusoma hotuba ya Katibu Charles Hinga amesema takwimu hizo zimetolewa katika taarifa ya hivi karibuni ya sekta na Principal Secretary Charles M. Hinga. Kwa mujibu wa hotuba hiyo, mpango huo kwa sasa unaendelea katika takriban kaunti 40, huku Serikali ikilenga kuufikisha katika kaunti zote nchini. Serikali pia imesema inalenga kuhakikisha kila eneo bunge kati ya 290 nchini linapata angalau nyumba 220, ikiwa sehemu ya mpango mpana wa kuongeza usambazaji wa nyumba za bei nafuu. Ku...