Mahafala 341 Wahitimu Kozi za utabibu katika Mahafali ya 19 ya chuo cha North Coast Medical Training College.
Jumla ya mahafala 341
wamefuzu katika vitengo mbalimbali katika taaluma ya utabibu na udaktari katika
chuo cha north coast medical training college katika mahafali ya 19.
Akiongea wakati wa hafla hiyo katibu mkuu wa chuo
hicho Ruben Waswa amesema chuo hicho kimeendelea kupiga hatua kubwa za
maendeleo, kikisajili ongezeko la idadi ya wahitimu kila mwaka kutokana na
ubora wa mfumo wake wa elimu na mafunzo.
Ameibainisha kuwa kozi za utabibu zinazotolewa na chuo
hicho zinawapa wahitimu fursa kubwa za kupata ajira kwa haraka nchini na katika
soko la kimataifa.
Aidha, amewahimiza wazazi na walezi kuwapeleka watoto wao katika vyuo vinavyotambuliwa na kutoa mafunzo bora ili kuwawezesha kupata elimu stahiki, kujiendeleza kitaaluma na kujenga mustakabali wenye mafanikio.
Kwa upande wake mwenyekiti wa Chama cha Shule
Binafsi nchini (KPSA), Rosebella Ojambo, amesema sekta binafsi ina jukumu
muhimu katika kupeana elimu ya matibabu kwa kuziba mapengo yaliyopo katika
mfumo wa elimu wa umma.
Amebainisha kuwa vyuo binafsi vya utabibu vinachangia kupunguza uhaba wa wataalamu wa afya nchini akitoa wito wa kuimarishwa kwa ushirikiano kati ya serikali na sekta binafsi ili kuhakikisha elimu bora inawafikia wanafunzi wengi zaidi.
Nae mmoja wa wakurugenzi wa chuo hicho Marriane Darwinkle Amewapongeza mahafala hao akiwa na Imani kuwa mafunzo na ujuzi waliopata utawawezesha kufanya kazi Kwa weledi sehemu yoyote ulimwenguni na kutoa mchango chanya katika kuboresha huduma za afya na kusaidia jamii
.jpeg)

.jpeg)

Comments
Post a Comment