MOMBASA MEGA MARATHON YAZINDULIWA, ZAIDI YA WASHIRIKI 1,000 WATHIBITISHA USHIRIKI WAO.

 

                                  

Mashindano ya Mombasa Mega Marathon yanatarajiwa kufanyika Jumapili, Agosti 16, baada ya kuidhinishwa na Shirikisho la Riadha nchini.

Makamu wa Kwanza wa Rais wa shirikisho hilo, Paul Mutwii, amezindua mashindano hayo jijini Mombasa Jumatatu, akimwakilisha Rais wa shirikisho hilo Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei.

Mutwii amesema wamefurahishwa na kurejea kwa mashindano makubwa ya Marathon Mombasa, baada ya kutokuwepo kwa miaka kadhaa.

                                 

Amesema Rais wa huyo amesaini kibali cha mashindano hayo, huku waandaaji wakitarajiwa kukabidhiwa kibali hicho wakati wa uzinduzi.

Mashindano hayo yatakuwa na mbio za kilomita 42, kilomita 21, kilomita 10 na kilomita 5.

Balozi wa Mombasa Mega Marathon, Omar Said, amesema zaidi ya washiriki 1,000 tayari wamejisajili kwa mashindano hayo ya kwanza.

Mbio za burudani za kilomita 5 zinatarajiwa kuanza kati ya saa mbili na nusu na saa tatu asubuhi.

                                     

Said amesema mbio hizo za burudani zinalenga watoto, wazee, familia na washiriki wengine ambao hawawezi kukimbia umbali mrefu.

Kwa mujibu wa Shirikisho la Riadha Nchini, jumla ya shilingi milioni 5.084 zimetengwa kama zawadi kwa washindi.

Wanariadha watakaoshinda zawadi watafanyiwa vipimo vya matumizi ya dawa zilizopigwa marufuku kabla ya fedha zao kutolewa.

Vipimo hivyo vitaendeshwa na Wakala wa Kitaifa wa Kupambana na Matumizi ya Dawa za Kulevya, ADAK.

                                   

Said amesema mbio  hizo inalenga pia kuhamasisha jamii ya Mombasa kupinga matumizi ya dawa za kulevya.

Akiongeza kuwa  waandaaji wanatarajia kusaidia makundi yanayofanya kazi na watu walioathirika na matumizi ya dawa za kulevya, kwa kushirikiana na mashirika kama Reachout na Mewa Rehabs.

Naibu Gavana wa kaunti ya Mombasa, Francis Thoya, amesema michezo inatoa fursa ya kukabiliana na tatizo la matumizi ya dawa za kulevya miongoni mwa vijana.

Thoya akisema Mombasa inakabiliwa na changamoto kubwa ya matumizi ya dawa za kulevya, akieleza kuwa vijana wasio na shughuli za kufanya huwa katika hatari kubwa ya kujiingiza katika matumizi ya dawa za kulevya na matatizo mengine ya kijamii.

                                 

Akisema kuna haja ya kuinua hadhi ya riadha Mombasa na kurejesha enzi ambazo jiji hilo lilikuwa mwenyeji wa mashindano makubwa ya riadha.

Kaunti ya Mombasa itasaidia mashindano hayo kwa kutoa usalama na huduma nyingine muhimu.

Afisa wa kiufundi wa Shirikisho la Riadha Nchini, James Mwaringa, amesema Bustani ya Mama Ngina Waterfront itakuwa eneo la kuanzia na kumalizia mashindano hayo.

Eneo hilo pia litatumika kama Race Village, ambapo shughuli mbalimbali za mashindano zitafanyika.

 

 

 

Comments

Popular posts from this blog

Viongozi wa Kidini PPRL Waunga Mkono Agizo la wizara ya elimu la Ratiba ya Masomo Shuleni

Mbunge Feisal Bader Atuhumiwa Kuzuia Msambweni Talent Show Kufanyika Mvindeni Youth Centre.

Kaunti ya Wajir yaandaa Sherehe za Madaraka Day kwa mara ya kwanza tangu Kenya ipate Uhuru.