MOMBASA MEGA MARATHON: KITUNDU NA CHERUIYOT WASHINDA MBIO ZA KILOMITA 42.

                           

Mwanariadha Little Nick Kitundu ameibuka mshindi wa mbio za kilomita 42 katika Mombasa Mega Marathon, baada ya kutumia muda wa saa 2:16:02.

Kitundu alifuatwa na Gabriel Kahora, aliyemaliza katika nafasi ya pili kwa muda wa  saa 2:18:39, huku Theophilus Kipsang akimaliza wa tatu kwa muda wa saa 2:18:54.

Kwa upande wa wanawake katika mbio za kilomita 42, Betty Cheruiyot alitwaa ushindi kwa muda wa saa  2:36:09. Akifuatwa na Lucy Chelele, aliyemaliza wa pili kwa muda wa saa  2:40:59, huku Anastacia Jepkoech akishika nafasi ya tatu kwa muda wa saa 2:42:27.

Katika mbio za kilomita 21 upande wa wanaume, Justus Muasya alishinda kwa muda was aa 1:00:52, akifuatiwa na Elisha Kipsoi aliyemaliza wa pili kwa muda wa saa 1:02:55 nae Tom Mwendwa Mutie akishika nafasi ya tatu kwa muda wa 1:05:57.

Akizungumza baada ya ushindi wake, Little Nick Kitundu amesema mbio hizo hazikuwa rahisi kutokana na hali ya hewa ya joto, lakini amefurahia kufanikiwa kushinda. Akisema  alifurahishwa na mazingira tambarare ya Mombasa, kwani amezoea kukimbia katika maeneo yenye milima na mabonde.

                                   

Kwa upande wake, Betty Cheruiyot amesema hali ya hewa ilikuwa changamoto kubwa, lakini haikumzuia kufanya vizuri na kutwaa ushindi.

Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya Mombasa Mega Marathon, Charles Omoto, ameipongeza Kaunti ya Mombasa kwa ushirikiano wake katika kufanikisha mbio hizo. Omoto akisema waandalizi wanapanga kufanya mashindano hayo kuwa ya kila mwaka, kutokana na vipaji vingi vilivyojitokeza.

Waziri wa Ardhi na Mipango ya Jiji katika Kaunti ya Mombasa, Mohamed Husein Amadoh, amewataka vijana kujiepusha na matumizi ya dawa za kulevya na badala yake kujikita katika michezo kama njia ya kuimarisha afya na kujenga maisha bora.

                                     

Amadoh amesema Mombasa Mega Marathon haikuwa tukio la michezo pekee, bali pia ilikuwa jukwaa la kuhamasisha umoja, maisha yenye afya na kujenga kizazi kisichotumia dawa za kulevya. Amewataka vijana kutumia fursa zinazopatikana kupitia michezo kugundua na kuendeleza vipaji vyao, kutafuta fursa za maendeleo na kufanya maamuzi yenye manufaa kwa maisha yao.

Gavana wa Kaunti ya Mombasa, Abdulswamad Sharif Nassir, amewapongeza waandalizi wa mbio hizo akisema wametanya kazi nzuri katika kuwasaidia vijana kujiepusha na matumizi ya dawa za kulevya na kujenga maisha bora kupitia hamasa yao.

Gavana Nassir amesema mbio hizo pia zimechangia pakubwa katika kukuza na kutangaza utalii wa kaunti ya Mombasa kupitia maonyesho ya maeneo mbalimbali ya kaunti hiyo.

Aidha, amewataka wanasiasa kujiepusha na kauli zinazoweza kuathiri sekta ya utalii, akisema kuathirika kwa utalii kunaweza kudhoofisha uchumi na kusababisha Wakenya wengi kukosa ajira.

                                    

Gavana Nassir amesema serikali ya kaunti itaendelea kuboresha mbio hizo ili ziwe kubwa, za kuvutia na zenye manufaa zaidi katika miaka ijayo.

Akiweka wazi kuwa  Mombasa imepiga hatua kubwa katika sekta ya michezo, huku viwanja vya kisasa vikiendelea kujengwa ili kuendelea kutambua na kukuza vipaji.

Mshindi wa mbio za kilomita 42 amejishindia zawadi ya shilingi 500,000, mshindi wa pili shilingi 250,000, huku mshindi wa tatu akipata shilingi 125,000. Zawadi zilitolewa hadi kwa mshindi wa nafasi ya kumi

Comments

Popular posts from this blog

Viongozi wa Kidini PPRL Waunga Mkono Agizo la wizara ya elimu la Ratiba ya Masomo Shuleni

Mbunge Feisal Bader Atuhumiwa Kuzuia Msambweni Talent Show Kufanyika Mvindeni Youth Centre.

Kaunti ya Wajir yaandaa Sherehe za Madaraka Day kwa mara ya kwanza tangu Kenya ipate Uhuru.